THANK YOU FOR VISITING #MaPROMO BLOG - WHERE WE KEEP IT BRIEF TO THE POINT AND CUT THE BS

THE MOVEMENT

THE MOVEMENT

Sunday, April 17, 2016

ALL WE NEED IS PRAYERS NOW..ANDREW SANGA TUKO PAMOJA #LIFE








**TAARIFA YA AJALI YA KAKA ANDREW SANGA**

Ndugu Wanajumuiya,

Kama ambavyo tumesikia kwenye mitandao asubuhi hii ya leo ndugu yetu Andrew Sanga (Drew) amepata ajali ya kupigwa risasi. Kesi bado iko mikononi mwa polisi na tutatoa taarifa rasmi ya tukio pindi tutakapopata habari kamili.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia Bw. Prosper Kiswaga hali ya Andrew siyo nzuri na kwasasa yupo ICU hospitali ya Memorial Hermann Southwest , 7600 Beechnut St, Houston, TX 77074

Kwa mujibu wa Bw. Kiswaga , madaktari wanashauri kusiwe na mkusanyiko mkubwa wa watu hospitalini hapo hadi hali ya ndugu yetu Andrew itakapotengamaa.

Mama mtoto wa Andrew , Bi. Emmy Matafu ( Mama Zoe ) yupo hapo hospitali kwenye chumba maalumu na tunaweza kwenda kumfariji na kumpa nguvu katika kipindi hiki kigumu.


Ndugu Wanajumuiya, Andrew Sanga anahitaji maombi yetu katika kipindi hiki ili aweze kuvuka salama katika mtihani huu na hatimaye kuungana tena na familia yake

Kila mtu kwa imani yake tumuombee kaka Andrew.

Taarifa zaidi zitawajia kila zitakapopatikana

Ahsanteni

Cassius Pambamaji
Msemaji wa THC

Powered by #MaPROMO BLOG - A Division of J & P ENT - All Rights Reserved